Wednesday 11 May 2016

WEST HAM: MASHABIKI WALIOVAMIA NA KUTUPA CHUPA KWENYE BASI LA MANCHESTER UNITED KUFUNGIWA MAISHA


Uongozi wa timu ya West Ham United imesema itawafungia maisha waliohusika na shambulizi la chupa na mawe kwenye basi la Manchester United jana...


Basi la Manchester United wakati linaelekea uwanjani lilikutana na umati wa mashabiki wa West Ham na mashabiki hao walianza kutupa chupa na vitu vingine kwenye basi hilo...


Ilikuwa hali ya hatari na polisi ilibidi waingilie kati na kuwasindikiza wachezaji hao...Uingereza zamani ilikuwa maarufu sana kwa vurugu za mashabiki wa mpira...


Neno hooliganism lilikuwa linatumika sana lakini miaka ya hivi karibuni uuni huo umepungua sana na vurugu za jana ziliamsha hisia za miaka iliyopita...Bofya hapa upate habari zaidi.

No comments:

Post a Comment