Sunday 31 August 2014

EPL: MSIMAMO WA LIGI MPAKA SASA

PositionTeamPlayedGoalDifferencePoints
No movement1Chelsea379
No movement2Swansea359
No movement3Tottenham256
No movement4Man City336
No movement5Arsenal214
No movement6Southampton314
No movement7Hull214
No movement8Aston Villa214
No movement9Stoke304
No movement10West Ham3-13
No movement11Liverpool2-13
No movement12QPR3-43
No movement13Sunderland3-12
No movement14Man Utd3-12
No movement15Newcastle3-22
No movement16Everton3-32
No movement17West Brom3-32
No movement18Leicester2-21
No movement19Crystal Palace3-31
No movement20Burnley3-31

EPL: CHELSEA YANG'OA KISIKI KIGUMU


Kama ulikosa game ya jana itabidi uangalie magoli hapo chini maana ilikuwa game kali sana kati ya timu 2 kali...Chelsea iliweza kuifunga Everton 6-3 katika mchezo ambao ulishangaza mashabiki hata watangazaji walishangaa jinsi mabao yalivyokuwa yanafungwa...


Chelsea walianza kufunga magoli mapema sana na ilitumika sekunde 35 tu wakati Cesc Fabregas alipompasia Diego Costa na kutingisha nyavu...Dakika ya 3 Ivanovic nae alipachika bao ambalo kwa utaalam wa soka ilikuwa offside lakini macho ya linesmen hayakuona vizuri...


Everton walipambana na kucheza vizuri sana lakini Chelsea walikuwa makini kulinda lango mpaka dakika ya 45 Mirallas alipofanikiwa kupata bao...Eto'o nae aliingia kama sub kwa mara ya kwanza toka ahamie Everton na mara ya kwanza kugusa mpira bao likapatikana...Katika historia ya premiership hii mechi ni ya 7 kwa magoli mengi kufungwa...Bofya hapa upate habari zaidi.


Saturday 30 August 2014

VPL: MALALAMIKO RASMI YA YANGA KUHUSU OKWI


Vita imepamba moto baada ya Yanga kusema Okwi bado ni mchezaji wao...Endelea kusoma hii barua malalamiko rasmi ya Yanga kwenda kwa TFF...


 TFF wasipotekeleza Yanga itapeleka issue FIFA na Mahakama ya usuluhisho....


VPL: MANJI ASEMA OKWI BADO NI WA YANGA


Yusuf Manji mwenyekiti wa Yanga akiwa na makamu mwenyekiti Clement Sanga waliitisha mkutano na waandishi wa habari na kutangaza Okwi bado ni mchezaji wa Yanga...Hii imetokea baada ya Simba kumtangaza Okwi kama mchezaji wao alhamisi na kwamba ataingia kambini rasmi...Uongozi wa Yanga umeshawaandikia TFF ili wawawekee vikwazo Simba na Okwi kwa kukiuka mkataba na pia wanataka fidia ya dola za 200,000...Manji amesema Yanga imewapa TFF siku 7 kushughulikia hili suala amasivyo watalipeleka FIFA na mahakama ya usulihishi...Bofya hapa upate habari zaidi.

EPL: RATIBA YA MECHI ZA LEO (GMT)

12:45              BurnleyBurnley v. Manchester United Manchester United
15:00             Manchester CityManchester City v. Stoke City Stoke City
15:00             Newcastle UnitedNewcastle United v. Crystal Palace Crystal Palace
15:00             Queens Park RangersQueens Park Rangers v. Sunderland Sunderland
15:00             Swansea CitySwansea City v. West Bromwich Albion West Bromwich Albion
15:00             West Ham UnitedWest Ham United v. Southampton Southampton
17:30             EvertonEverton v. Chelsea Chelsea

EPL: AC MILAN WAMCHUKUA TORRES KWA MKOPO


Chelsea striker Fernando Torres anaingia AC Milan kwa mkopo...Chelsea wamemuachia aende huko kutokana na matakwa yake na pia kikosi kinavifaa vipya kama Diego Costa kwahiyo hawamhitaji...Torres alihamia Chelsea kwa pesa nyingi sana (pounds milioni 50) lakini hakuweza kulinganisha kiwango chake na hizo pesa...Mkopo ni wa miaka 2 na sasa anasubiri kukubaliana na masharti na kupita uangalizi wa madaktari...Bofya hapaa upate habari zaidi.

Thursday 28 August 2014

CAMEROON: ETO'O ASTAAFU INTERNATIONAL FOOTLBAL


Samuel Eto'o ametuma ujumbe kwenye Instagram yake akisema ameachana na soka la kimataifa na anawashukuru waafrika na mashabiki wake wote duniani kwa support aliyopata...Eto'o hato cheza kwenye AFCON January na atakuwepo muda wote na timu yake mpya ya Everton...Eto'o ameshachezea timu kubwa sana kama Real Madrid, Barcelona, Chelsea na nyingine...Alianza mechi za kimataifa 1997 wakati walivyo chapwa na Chile 5-0...Bofya hapa upate habari zaidi...

CHAMPIONS LEAGUE: GOLI LA KWANZA LA ALEXIS SANCHEZ LAIPELEKA ARSENAL GROUP STAGE


Arsenal sasa inaingia group stage ya Champions League mara ya 17 mfululizo na goli la kwanza la Alexis Sanchez ndilo lililoipeleka Arsenal mbele...Game ilikuwa ngumu kwa Arsenal hasa mwishoni ukizingatia walibaki 10 baada ya Mathieu Debuchy kutolewa nje...


Beki ya Arsenal ilikuwa imara maana kuna wakati presha za mashibiki wengine zilianza kupanda...Arsenal waliwakosakosa Besiktas lakini hawakuweza kuongeza magoli...Sanchez aliweza kutingisha nyavu dakika ya 45 na ndio goli pekee la usiku huo...Besiktas walilalamika kunyimwa penalty wakati Ramon Motta alipokwatuliwa na Jack Wilshere ndani ya 18...


Kutokana na Giroud kuvunja mguu na anaweza asicheze mpaka mwakani inabidi Wenger achangamkie mchezaji mwingine kabla ya dirisha la usajli halijafungwa...Bofya hapa upte habari zaidi.

Wednesday 27 August 2014

EPL: ETOO NDANI YA EVERTON


Samuel Eto'o ameingia Goodison Park rasmi...Amesaini mkataba wa miaka 2...Eto'o alikuwa Chelsea na baada ya mkataba wake kuisha timu ya Martinez imemchukua na iko tayari kutumia ujuzi wake...Ameshapitishwa na madaktari na sasa yuko tayari kwa mechi ya jumamosi dhidi ya timu yake ya zamani...Bofya hapa upate habari zaidi..

NBA: HASHEEM THABEET ACHUKULIWA NA SIXERS


Hasheem Thabeet mtanzania anayecheza mpira wa kikapu wa kulipwa kwenye ligi ya NBA amechukuliwa na Sixers....Thabeet alikuwa Oklahoma Thunder na athamia Sixers kwa makubliano ya cash na pia issue za draft pick ijayo...Lakini inasemekana hatokaa sana Sixers...Kwa habari zaidi Bofya hapa. 

CAPITAL ONE CUP: MK DONS YAIAIBISHA MANCHESTER UNITED


MK Dons au Milton Keynes Dons Football Club ka timu ambako kako madaraja mawili chini ya Manchester United jana waliiaibisha Manchester United mbele ya mashabiki 26,969...MK Dons walicheza mpira safi na waukweli wakiwaacha Man United wakitoa macho na kushangaa tu wakati mabao 4 yanaingia...Timu hii imeundwa mwaka 2004 kwa hiyo ina miaka 10 tu ukilinganisha na wakongwe Manchester United ambao wapo toka 1878...Will Grigg alipachika la kwanza dakika ya 25 kutokana na kosa la Johnny Evans...Pia kipindi cha pili huyo huyo Grigg alipachika bao la kifuani la dakika ya 63...Dogo ambae yuko MK kwa mkopo Benik Afobe alipachika mabao yaliyobaki...Bofya hapa  upate habari zaidi.

Tuesday 26 August 2014

DAR-ES-SALAAM WEEKEND RIDES CLUB: WADAU TUJIUNGE NA HII CLUB, MAZOEZI MUHIMU SANA.

DWRC wakiwa Kinondoni Morocco tayari kwa safari...

Dar es Salaam Weekend Rides Club chini ya uongozi wa Emmanuel N. M. Manase ni club ya kuendesha baiskeli ambayo inakuwa na ruti kutoka Kinondoni Morocco mpaka Bahari Beach siku za weekend...


DWRC wakipata break ya matikiti maji katikati ya safari...
Karibuni wadau wa Max Sports tujitokeze tufanye mazoezi mara kwa mara...


Njia panda ya Kunduchi (Mbuyuni) ni sehemu ya kusubiri wengine...

Club hii ni muhimu sana katika kuimarisha afya na akili pia...


Budget Bahari Beach wakipumzika...


Wadau wa DWRC wamefika Bahari Beach Hotel (Ledger Plaza) salama...



Time ya kupumzika kidogo sasa...
Bahari Beach Hotel (Ledger Plaza)

Karibuni wadau wote...


EPL: LIVERPOOL CHALI ETIHAD STADIUM


Liverpool jana ilikumbushwa kwamba soka lazima usifanye makosa nyuma...Kosa la Alberto Moreno nyuma lilisababisha bao la kwanza kutoka kwa Stevan Jovetic...Kipindi cha kwanza kama dakika 40 hivi Liverpool walicheza vizuri na kufika golini kwa Man City mara kwa mara lakini hawakuweza kutengeneza bao...Baada ya kuchapwa dakika ya 41 Man City waliwapeleka shule Liverpool wakati Mario Balotelli akiangalia timu yake ya zamani ikiwashughulikia timu yake mpya...


Dakika ya 55 huyo huyo Jovetic aliandika bao la 2...Sergio Aguero aliingia kipindi cha 2 na baada ya sekunde 23 alitingisha wavu...Dakika ya 83 Liverpool wakazawadiwa goli la bure na Pablo Zabaleta...Man City ni kazi kama kawa ila Liverpool inabidi wajipange nyuma na wamtumie Balotelli vizuri...Bofya hapa upate habari zaidi.

Monday 25 August 2014

EPL: DI MARIA AMESHAAGA WACHEZAJI WENZAKE REAL MADRID


Tetesi kuwa Manchester United wako mbioni kumchukua Di Maria sasa zimethibitishwa na Carlo Ancelotti...Ancelotti amesema Di Maria alikuja club lakini hakufanya mazoezi alikuja kuaga wenzake...Bado mambo hayajawekwa hadharani lakini inasemekana wamekubaliana dau la pound milioni 64 na sio milioni 75 ambayo Real walikuwa wanataka...Van Gaal amesema hatozungumzia transfer yoyote mpaka itapokamilika...Van Gaal anahitaji sana kuimarisha kikosi chake ambacho kwa sasa kinayumba vibaya...Bofya hapa upate habari zaidi.

EPL: MANCHESTER UNITED HOI STADIUM OF LIGHT


Manchester United bado wako chini ya kiwango na game ya jana ilidhihirisha hiyo...Manchester United walitoka sare 1-1 na Sunderland katika game ambayo Sunderland ndio walionekana timu bora zaidi...Mata alipata bahati na deflection ya beki wa Sunderland akafanikiwa kufunga bao lakini baada ya nusu saa uzembe wa mabeki wa Manchester ulimwezesha Seb Larsson kupiga cross iliyomkuta Jack Rodwell na kichwa chake kikafunga bao safi...Ashley young alipigwa kadi kwa kupiga mbizi lakini inavyookana kwenye re-play kaonewa kiaina lakini pamoja na hayo refa alipeta sana issue za Man...Van Gaal alisema itakuwa miujiza Manchester United kuchukua ubingwa kwa hali hii...Bofya hapa upate habari zaidi.

EPL: MSIMAMO WA LIGI MPAKA SASA

PositionTeamPlayedGoalDifferencePoints
No Movement1Tottenham256
No Movement2Chelsea246
No Movement3Swansea226
No Movement4Arsenal214
No Movement5Hull214
No Movement6Aston Villa214
No Movement7Man City123
No Movement8West Ham213
No Movement9Liverpool113
No Movement10Everton202
No Movement11Sunderland202
No Movement12West Brom202
No Movement13Man Utd2-11
No Movement14Southampton2-11
No Movement15Stoke2-11
No Movement16Leicester2-21
No Movement17Newcastle2-21
No Movement18Crystal Palace2-30
No Movement19Burnley2-30
No Movement20QPR2-50