Tuesday 30 September 2014

CRICKET: REKODI YAVYNJWA JUU YA MLIMA KILIMANJARO


Rekodi mpya ya dunia imewekwa baada ya timu ya Cricket yenye international stars wa zamani kucheza mchezo huo juu ya mlima Kilimanjaro na kuwa mechi ya kwanza kuchezewa katika altitude ya juu sana...


Mechi hiyo ilichezewa eneo ambali liko chini kidogo ya summit kwenye eneo la crater ambalo liko flat na ni urefu wa mita 5,730 (18,799ft) kutoka uwasa wa bahari...


Walicheza 10 overs kila moja Twenty20 mpaka mawingu yalipowafunika...Bofya hapa upate habari zaidi.


EPL: PARDEW WA NEWCASTLE MAJI SHINGONI


Newcastle yapoteza mechi nyingine dhidi ya Stoke City baada ya Peter Crouch kupachika bao...Kifaa cha Newcastle Papiss Cisse alikuwa benchi kwenye mechi hiyo dhidi ya Stoke na akaingizwa kiaina badae...Allan Pardew kocha wa Newcastle sasa presha inapanda kwani hana ushindi hata 1 katika mechi 6 za premiership...

Habari ndio hiyo kutoka kwa mashabiki wa Newcastle...
Stoke ndio kwanza wanapata ushindi wao wa 1 nyumbani...Hali ni tete kwani pia Newcastle msimu uliopita walishinda mechi 25 tu na sasa hasira za mashabiki zimeanza kumgeukia kocha na asipoibadili timu na kuanza kushinda atajikuta nje ya uwanja...Bofya hapa upate habari zaidi.

Monday 29 September 2014

VPL: YANGA YAWAKIMBIZA WAJELAJELA


Yanga imefanikiwa kuchukua points 3 baada ya kuichapa Magereza almaaruf kwa jina la Prisons au Wajelajela 2-1...Mechi ilikuwa kali sana na pande zote zilistahili pongezi kwa kujituma na kucheza soka safi....Huu ni ushindi wa 1 kwani walishindwa kuchukua points 3 mechi yao ya kwanza dhidi ya Mtibwa Sugar au Wakata Miwa...


Yanga ndio walioanza kuona lango la mwenzie baada ya Mrisho Ngasa kufanyiwa ndivyo sivyo na refa akatoa free-kick...Dead ball ilipigwa na mchezaji mpya wa Yanga kutoka Brazil Andrey Coutinho na kuwanyanyua mashabiki wa Yanga baada ya kupachika bao hilo dakika ya 34...Bofya hapa upate habari zaidi.

LA LIGA: MESSI HAKUAMINI KAMA ANGEFIKISHA MAGOLI 400


Mabao 400 si mchezo lakini Lionel Messi mwenye umri w miaka 27 sasa amefikisha mabao 401 kwa kuchezea Barcelona na nchi yake ya Argentina...Messi hakuamini kama angefikia mabao 400 alifikia magoli 400 kwenye mechi ya Barca dhidi ya Granada FC ambapo walishinda 6-0 na yeye alikuwa na mabao 2 katika hiyo mechi...Mabao 359 kaifungia Barcelona na 42 Argentina...Messi ni kati ya wachezaji bora wa soka duniani...Bofya hapa upate habari zaidi.

EPL: MATOKEO YA MECHI ZA WEEKEND

Sunday 28 September 2014

SHENZEN OPEN: ANY MURRY WINS THE SHENZEN TITLE


Andy Murry has beaten Tommy Robredo to lift the Shenzen Open in China.
 

VPL: SIMBA YAKWAA KISIKI TENA

Shaban Kisiga wa Simba akifukuzia mpira...
Wana Msimbazi Simba SC wameshindwa kunyakua points 3 kwa kutoka sare na Police ya Morogoro 1-1...Kikosi kilikuwa hakina kipa wao hodari Ivo Mapunda na mchezaji mpya Raphael Kiongera kwasbabu ni majeraha...Kipa Hussein Shariff alichezeshwa pamoja na mabeki Chollo na Mohamed Hussein...Simba walicheza vizuri midfield lakini kipindi cha 2 Police walikuwa moto zaidi kupitia Danny Mrwanda na Christopher Edward wakisaidiwa na Salum Machaku ambao walikuwa wachezaji wa zamani wa Simba waliweza kusababisha bao kupitia kwa Mohamed Adolf dakika ya 50...Bofya hapa upate habari zaidi.

LA LIGA: MSIMAMO WA LIGI MPAKA SASA

PositionTeamPlayedGoalDifferencePoints
No movement1Barcelona61716
No movement2Atl Madrid6714
No movement3Valencia51113
No movement4Sevilla6213
No movement5Real Madrid61112
No movement6Celta de Vigo6412
No movement7Villarreal618
No movement8Eibar618
No movement9Rayo Vallecano608
No movement10Granada CF6-58
No movement11Málaga5-26
No movement12Espanyol5-15
No movement13Almería5-15
No movement14Real Sociedad5-14
No movement15Ath Bilbao6-24
No movement16Deportivo de La Coruña5-74
No movement17Elche6-94
No movement18Levante6-114
No movement19Getafe5-83
No movement20Córdoba5-72

LA LIGA: BARCA YAISAMBARATISHA GRANADA


Msimu mpya unaenda vizuri kwa timu ya Barcelona baada ya kuibugiza Granada FC mabao 6-0...Dogo Neymar, Jr alifanikiwa kurudi nyumbani na mpira baada ya kupata hat-trick kwenye hiyo game...Lionel Messi alipata mabao 2 na Rakitic bao 1...Kocha mpya Luis Enrique ambaye alichukua timu kutoka kwa kocha kutoka Argentina Gerardo "Tata" Martino sasa amefanikiwa kuimarisha kikosi na wakiendelea na hii kasi ubingwa utapatikana mapema sana...Bofya hapa upate habari zaidi.




EPL: MATOKEO YA MECHI ZA JANA

Friday 26 September 2014

GET TO KNOW THE BEST DRIBBLER AND SOCCER MAGICIAN | GARRINCHA


Manuel Fransisco dos Santos is also popularly known as Garrincha (a small bird) was a very skillfull soccer player and dribbler of  the bygone era but up to now he is considered the best in the history of soccer

EPL: RATIBA YA MECHI ZINAZOKUJA (GMT)

SAT 27 SEP 2014 - PREMIER LEAGUE
  • LiverpoolvEverton12:45
  • ChelseavAston Villa15:00
  • Crystal PalacevLeicester15:00
  • HullvMan City15:00
  • Man UtdvWest Ham15:00
  • SouthamptonvQPR15:00
  • SunderlandvSwansea15:00
  • ArsenalvTottenham17:30
SUN 28 SEP 2014 - PREMIER LEAGUE
  • West BromvBurnley16:00
MON 29 SEP 2014 - PREMIER LEAGUE
  • StokevNewcastle20:00

Thursday 25 September 2014

GHANA: ASAMOAH GYAN AZUSHIWA KUUA RAFIKI


Ghanaian international football star Asamoah Gyan amezushiwa kumuua rafiki yake wa karibu sana na kutumia mwili wake kwa issue za kishirikina...Gyan alichukua rafiki zake kama 16 wakaenda kusini mwa Ghana sehemu inaitwa Ada kwa mapumziko mafupi...Walivyokuwa huko Ada Theohillus Tagoe maarufu sana Ghana kwa jina la Castro na pia ni mwimbaji wa nyimbo za Hiplife au Afrobeat alimchukua rafiki yake wa kike, Janet Bandu, wakaenda kupanda pikipiki za majini au kwa jina jingine Jet Ski...


Baada ya hapo hakuna mtu aliwaona tena na Gyan na rafiki zake wakisaidiwa na Police waliwataafuta sana bila mafanikio...Sasa police wanasema Castro na mwenzake wakakuwa wamefariki...Vyombo vya habari huko Ghana vinasema Gyan alimuua mwenzake iliafanye mambo ya kishirikina ili aendelee kufanikiwa...Gyan na familia yake imekanusha kuhusika na kifo chake na wameongea na waandishi wahabari kuhusina na hili suala...Hapo chini ni moja video ya maarufu ya Castro akiwa na rafiki yake Gyan...Bofya hapa upate habari zaidi.


EPL: NEWCASTLE'S JONAS GUTIERREZ'S CANCER HAS PREAD


Newcaste midfielder Jonas Gutierrez is suffering from testicular cancer.
 

CAPITAL ONE CUP: MAN CITY YAFANYA KWELI

Mchezaji mpya wa City
Jose Angel Pozo akipachika bao la 6...
Manchester City imesambartisha na kuigaragaza Shefield mabao 7 kwa mtungi (0)...Magoli yote yalipatikana kipindi cha 2...Frank Lampart alipokea cross kutoka kwa James Milner na kufungua dimba...Dzeko na akafuata baada ya pasi safi kutoka kwa Navas na bao la 3 lilitoka kwa Jesus Navs...Kamil Zayate alimkwaa Frank Lampard na City wakapewa penalty dakika ya 60 na Yaya Toure hakufanya kosa na bao la 4 likaandikwa ubaoni...Bofya hapa upate habari zaidi.

Wednesday 24 September 2014

NBA: DERRICK ROSE ATOA DOLA MILIONI 1 KUSAIDI WATOTO WASIOJIWEZA


Star wa Chicago Bulls Derrick Martell Rose ametoa dola milioni 1 kusaidia program za watoto waishio katika mazingira magumu baada ya kutoka shule...Ametoa pesa hizo kwenye NGO inayosaidia watoto wanaoishi kwenye umaskini huko Chicago Marekani...Derrick ni mchezaji aliyetoka kwenye mazingira magumu na kujitahidi mpaka amekuwa tajiri na mchezaji hodari sana wa Basketball...Hapo chini ni press release yake...Safi sana Derrick kwa kuonyesha mfano mzuri...

“To have a strong community of people who believe in your potential can make all the difference in the world,” said Rose, a native of Englewood, who is a point guard for the Chicago Bulls. “So many people have invested in me and I want to do the same for Chicago’s teens.”


NFL: JASON PETERS WA EAGLES ASEMA ATAMGONGA TENA MTU ANAYEMZENGUA QB


Jason Peters offensive tackle wa Eagles alitolewa kwenye game ya Philadelphia Eagles na Washington Redskins baada ya kumvaa Chris Baker wa Redskin...Peters alimvaa Bakers kwasababu QB wa Eagles Nick Foles alifanyiwa foul mbaya na baada ya hapo kulikuwa na commotion ya wachezaji wakitaka kuzichapa...Bofya hapa upate habari zaidi.


CAPITAL ONE CUP: LIVERPOOL NA MIDDLESBROUGH YASAWAZISHA HISTORIA

Supper Mario akipiga penalty...
Liverpool na Middlesbrough wafikia rekodi ya penalties baada ya mechi kuisha 2-2...Zilichapwa penalties 30 mbele ya the Kop zikiwaacha mashabiki wakishangaa na kutoa macho balaa...Baada Albert Adomah wa Middlesbrough kukosa penalties Liverpool walisoga mbele...

Albert akikosa penalty iliyowapeleka Liverpool mbele...
Liverpool waliongoza mapema kipindi cha 1 kupitia kwa Rossiter na Middlesbrough walisawazisha kipindi cha 2 na mpira ukafika dakika za nyongeza ndipo Suso alipowaweka Reds mbele lakini penalty dakika za mwisho kabisa kupitia kwa Patrick Bamford ililazimisha shootout...Cheki hapo chini magoli yalivyoingia...Bofya hapa upate habari zaidi.