Thursday 31 March 2016

F1: ALONSO NJE BAHRAIN GRAND PRIX BAADA YA AJALI MBAYA SANA


Alonso hatoweza kushiriki Bhahrain GP baada ya kupata ajali mbaya sana...Alonso amevunja mbavu na pafu lake la kulia halifanyi kazi vizuri...Alipata ajali mbaya akiwa na spidi ya kilometa 180 kwa saa...


Madaktari wake wamsema hawatomruhusu kushiriki kutokana na majeraha yake na sasa dereva Stoffel atachukua uskani kwa mara ya kwanza kwa niaba ya McLaren...Bofya hapa upate habari zaidi.

Saturday 26 March 2016

CHELSEA: KIPA WA CHELSEA HASEMI KAMA ATABAKI AU LA


Thibaut Courtois amesema hajui kama atasaini mkataba mpya darajani...Kipa huyo mwenye umri wa miaka 23 yuko kwenye mechi za kikataifa na timu yake ya Ubelgiji...Ubelgiji watacheza na Portugal Jumanne na mechi itafanyika Leira baada masuala ya kigaidi kutokea Ubelgiji na kuua watu wengi... Baada ya Chelsea kutofanya vizuri msimu huu amekubali kuwa imembadilisha huku Real Madrid wakimnyemelea huyu dogo...Courtois alikuwa mchezaji wa zamani wa Genk timu ya Mbwana Samatta...Bofya hapa upate habari zaidi.

INTERNATIONAL FRIENDLIES: RATIBA YA MECHI ZA LEO (GMT)


  • Germany19:45England
  • Azerbaijan15:00Kazakhstan
  • Russia16:00Lithuania
  • Austria16:30Albania
  • Poland16:30Finland
  • Hungary17:00Croatia


Thursday 24 March 2016

INTERNATIONAL CHAMPIONS CUP: LEICESTER WATACHEZA NS BARCA NA PSG


Leicester wanaoongoz ligi ya EPL watacheza na Barcelona na Paris St-Germain kwenye michuano ya kabla ya msimu wa kawaida...Timu nyingine zitazoshiriki ni Chelsea, Tottenham, Manchester City na Liverpool...Bofya hapa upate habari zaidi.

Tuesday 22 March 2016

NCAA TOURNAMENT 2016: MARCH MADNESS NOMA BALAA


Kwa wapenzi wa Basketball duniani March Madness ni kitu cha kuangalia...March Madness ni kipindi ambapo shule za vyuo Marekani vinachuana vikali mwezi March...Sasa kilichotokea mwaka huu ni mambo ambayo hayakutegemewa kabisa...Kwanza, tuanze na timu ya shule ya wasongo darasani ya Yale...



Yale wamewatoa wakali Baylor ambao ni namba 5 kwa ukali...Pili, Wichita State ambao karibu wasicheze wamewatoa wakali Arizona ambao ni namba 6 kwa ukali...Tatu, Arkansas-Little Rock ambao wamechukua kocha wa mwaka wa kwanza wamewatoa namba 5 Purdue...


Nne, namba 15 Middle Tennessee wamewatoa namba 2 Michigan State ambao ndio walikuwa wanatarajiwa kufika mbali sana dah...Imekuwa kali ya mwaka huu....Tano, Syracuse katimu ambao hata kasingekuwa ndani ya michuano ya NCAA wamewachapa vibaya Dayton na MTSU na kutinga 16 bora...


Sita, Iowa walichapa Temple ambao wazuri tu...Saba, Hawaii nao kwa mara ya kwanza wamechida game ya NCAA...Ngoja niishie hapo hebu pata habari zaidi kwa kubofya hapa.

INTERNATIONA SCHOOL DAY: BQ YOUTH MABINGWA


Timu ya BQ Youth wamewachapa wenyeji wao Moro Kids bao 1-0...Bao lilitoka kwa kijana hatari sana uwanjani Habibu Kiyombo...Mechi hii hufanyika mara 1 kwa mwaka katika viwanja vya Morogoro International School (MIS)...Washiriki walikuwa Laureate International, Capstone Feza na Morogoro International School...Bofya hapa upate habari zaidi.

TENNIS: CEO WA INDIAN WELLS AMEACHIA NGAZI BAADA YA MATAMSHI YAKE YA KUKEJELI TENNIS YA WANAWAKE


CEO wa Indian Wells, Raymond Moore, ameachia ngazi uongozi wa Indian Wells baada ya matamshi ya kukejeli Tennis ya wanawake...More alisema tennis ya wanawake iko nyuma ya mkia wa makoti ya wanaume...Matamshi hayo yameonekana kama kejeli na United States Tennis Association (USTA) wamesema matamshi hayo ni ubaguzi wa kijinsia...Bingwa wa dunia kwa upande wa wanawake amesema matamshi ya Moore yanakasirisha na nio sawa...Bofya hapa upate habari zaidi.

Monday 21 March 2016

BOXING: ROY JONES JR AMESHINDA PAMBANO DHIDI YA SHABIKI


Roy Jones Jr. amezichapa na shabiki wake na kushinda pambano kwenye round ya 2...Kati ya mashabiki 1,500 waliotaka kuzichapa na Roy Jones Vyron Phillips aliibuka mshindi wa kura zilizopigwa Facebook...Angeshinda angepewa $100,000...Jones alisema hana issue yoyote mbeleni  baada ya kuchapwa na Enzo Maccarinelli mwaka jana...Bofya hapa upate habari zaidi.

INDIAN WELLS FINAL: VICTORIA AZARENKA AMEMTOA NJE SERENA WILLIAMS NA KUSHINDA KOMBE


Namba 1 duniani Serena Williams ametolewa kwenye michuano ya Indian Wells na Victoria Azarenka...Azarenka aliamua kukomaa alivyoona Serena hapigi serve zake vizuri na kushinda mechi 6-4 6-4...Kwa upande wa wanaume Novak Djokovic amemchapa Milos Raonic kutoka Canada 6-2 6-0 na kubeba taji la Masters kwa mara ya 27...Bofya hapa upate habari zaidi.

EPL: MSIMAMO WA LIGI MPAKA SASA

1Leicester312366
2Tottenham313261
3Arsenal301855
4Man City302051
5West Ham301250
6Man Utd301150
7Southampton31947
8Stoke31-346
9Liverpool29544
10Chelsea30441
11West Brom30-739
12Everton291038
13Bournemouth31-1238
14Watford30-237
15Swansea31-936
16Crystal Palace30-833
17Norwich31-2228
18Sunderland30-1926
19Newcastle30-2625
20Aston Villa31-36
16