Sunday 13 July 2014

BOXING: ALVAREZ AMTWANGA LARA


Canelo Alvarez ameshinda pambano lake dhidi ya Erislandy Lara kwa split decision.


Alvare a,maye alichapwa vibaya sana na Floyd Mayweather sasa amejifunza na amefanikiwa kushinda pambano ambalo alikuwa anatafutwa bingwa wa dunia wa junior middleweight.

Pambano hilo lilifanyika MGM Grand mbele ya mashabiki 14,239.

Lara ni mkali sana wa Southpaw lakini hakufua dafu mbele ya makonde mazito ya Alvarez.

Score card za majaji zilikuwa kama ifuatavyo Levi Martinez (117-111) Dave Moretti (115-113) na Jerry Roth (115-113). 

Ukumbi ulilupuka kwa kushangilia walivyosikia Alvarez katangawa mshindi.

Alvarez ni supa staa mkubwa sana Mexico...Bofya hapa upate habari zaidi...

No comments:

Post a Comment