Thursday 18 August 2016

RIO 2016: USA WAMEMALIZA 1, 2, 3 MBIO ZA 100M VIHUNZI


Team ya USA ya riadha za mbio za mita 100 za vihunzi (hurdles) wameshinda kwa kuchukua nafasi zote za juu kwa mara ya kwanza.


Brianna Rollins toka achomoke wa kwanza mwanzoni hakuachia mpaka mwisho na kubeba dhahabu.


Rollins alitumia muda wa sekunde 12:48 na kuongoza wenzake kutoka US na kuweka historia kuwa timu ya kwanza kufanya hivyo toka mashindani hayo ya mita 100 vihunzi kuanzishwa mwaka 1972.


Nia Ali alishinda Silver kwa muda wa sekunde 12: 59 na Kristi Castin alichukua Bronze kwa muda wa 12:61...Bofya hapa upate habari zaidi.

No comments:

Post a Comment