Wednesday, 11 June 2014

WORLD CUP 2014: BADO SIKU 1 TU MAMBO YAANZE KWENYE NCHI YA SAMBA


Bado siku 1 tu mambo yaanze huko Brazil...Mwaka huu tunatarajia kuona soka safi na pia tutaona timu tofauti zikishika nafasi nzuri mwaka huu...Msikose kuangalia...Hebu jipe nafasi kuifaham Group A hapo chini...Goup hii ni kali sana na hapo watabiri mseme wenyewe...Maana ni soo...


Group APPts
1.BrazilBrazil00
2.CroatiaCroatia00
3.MexicoMexico00
4.CameroonCameroon00

NBA: SAN ANTONIO WASHINDA GAME 3


Game 3 iliyoisha dakika chache zilizopita imechukuliwa na San Antonio Spurs 111-92...Toka kipindi cha kwanza Miani walikuwa nyuma kwa points mpaka mwisho wa game...Spurs leo wamevunja rekodi ya NBA ya Shooting Percentage ya 75.8% kipindi cha kwanza...


Pia Kawhi Leonard amepata career-high points 29...Miami leo wamekula vumbi  tu mpaka mwisho...LeBron James na Dwane Wade wote walipata points 22...

FIFA: SEPP BLATTER AAMBIWA AONDOKE MWAKANI



Boss wa FIFA ameambiwa atimke mwakani kwasababu matizo mengi sana FIFA ameyasababisha yeye...Hii ilisemwa na wadau wengi wa FIFA akiwemo Michael Van Praag ambaye ni raisi wa Shirikisho la Soka la Udachi ambaye alisema FIFA sasa hivi haichukuliwi kama Shirikisho makini na vyovyote unavyo angalia Sepp Blatter ndio sababu...Pia bosi wa Shirikisho la Mpira la Uingereza Greg Dyke ameshangazwa sana na jinsi Sepp alivyochukulia tuhueji ma za rushwa zinazohusu Qatar kupata nafasi ya kuwa mwenyeji wa World Cup...Bofya hapa upate habari zaidi...


Tuesday, 10 June 2014

EPL: ASTON VILLA YAMCHUKUA JOE COLE


Baada ya Aston Villa kumchukua beki wa zamani wa Arsenal Phillip Senderos sasa wanamchukua Joe Cole kwa free transfer na wanasubiri ushauri wa daktari...Joe Cole mwenye umri wa 32 ni midfielder mzuri na amechezea timu kubwa kama Liverpool, Chelsea na Lille kwa mkopo...Joe Cole anatarajiwa kuweka mambo sawa kwani midfield ya Aston Villa ilikuwa inapwaya...

Monday, 9 June 2014

TANZANIA FOOTBALL FEDERATION: GABRIEL 'GEBO' PETER KUZIKWA MOROGORO


Gebo Peter mchezaji mahiri wa miaka ya nyuma atazikwa kwao Kugurunyembe Morogoro...Gebo alifariki Muhumbili Alhamisi iliyopita...Habari hizi zilitolewa na msemaji wa TFF bwana Wambura na wamesikitishwa na taarifa za kifo hiki...Gebo alianza kuichezea Sigara SC miaka ya 90 mwanzoni...Gebo ametokea kwenye familia ya wanamichezo kwa mfano, Peter Tino, mchezaji wa timu ya taifa miaka ya 80 ambae alisaidia timu ya taifa kufuzu michuano ya African Cup of Nations (AFCON) 1980 ni kaka yake Gebo...Peter Tino ni kati ya wachezaji maafuru sana Tanzania na mchango wake katika soka hautosahaulika kamwe...Abubakar Kombo mchezaji aliyecheza na Gebo Sigara SC amesikitika sana na amesema ni pigo kwa soka ya Tanzania...Pumzika kwa Amani Gebo Peter...

F1: RICCIARDO ASHINDA GP YA CANADA KWA STYLE


Ricciardo ameyakua kombe la GP huko Canada baada ya kumpita Nico Rosberg wa Mercedes mwishoni wakati zimebaki laps 2...Ricciardo ambaye yuko timu ya Reb Bull alijitahidi sana baada ya Lewis Hamilton kutoka kutokana na matatizo ya brakes...Sasa Hamilton yuko nyuma ya Nico Rosberg kwa pointi 22...Mashindano haya ya Canada yalikuwa makali sana toka kona ya kwanza mpaka mwisho...Tumeona Massa akipata ajali mbaya sana ambayo ilisababishwa na Sergio Perez wakati wanashindana....
 
Ajali ya Massa iliyosababishwa na Perez

Perez alimgonga Massa na gari la Massa likakosa mwelekeo na kugonga kingo za pembeni...Perez amepewa adhabu na uongozi wa F1 kutokana na ajali hiyo...Massa na Perez walipelekwa hospitalini lakini wanaendelea vizuri sasa baada ya kuachiwa huru na madaktari....Bofya hapa upate habari zaidi...

FRENCH OPEN: NADAL BINGWA


Rafa Nadal (namba 1 duniani) amenyakua tena French Open huko Rolan Garos...Rafa alimchapa Djokovic (namba 2 duniani) katika mechi ambayo alianza akiwa anakimbizwa seti ya kwanza...Seti ya 2 Djokovic alianza kumwachia Rafa points za bure...Baada ya hapo Seti zinazofuata Raafa aliweza kumshinda mwenzake kwani Djokovic alikuwa anakosa serve zake za kwanza na pia alikuwa anakosea sana...Rafa alishinda kwa seti 3-6 7-5 6-2 6-4...Sasa Rafa ameshinda Grand Slam 14 na yuko chini ya Roger Federer kwa Grand Slam 3...Hii ni mara ya 9 anashinda hapo Ufaransa...Bofya upate habari zaidi...

WORLD CUP 2014: JAMAICA YALA KICHAPO KIKUBWA NA FRANCE

Karim Benzema akishangilia bao

Katika mechi za kupasha misuli na kujiweka tayari kwa World Cup ya mwaka huu ambayo itaanza siku 3 zijazo Jamaica imejikuta ikilambishwa magoli 8 na Ufaransa...Mtu wa kwanza kuona lango la Jamaica alikuwa Yahan Cabaye kutoka PSG ambaye alipokea pasi saafi kutoka kwa Olivier Girud wa Arsenal dakika kama ya 17 hivi...Kabla ya half-time Jamaica walikuwa chini mabao 3...Baada ya hapo ikaja mvua ya mabao tu....Ufaransa walisikitika mchezaji wao Mathieu Debuchy kuumia na inawezekana akakosa mechi ya ufunguzi...Bofya hapa upate habari zaidi...

NBA: LeBRON NA TIMU YAKE WASAWAZISHA MAMBO



Miami Heat wameweza kusawazisha series 1-1 baada ya kushinda game 2 huko San Antonio Marekani...Wakati huu timu zote zilikuwa zinacheza vizuri na LeBron aliibuka na point 35 na rebound 10...Bosh aliwaokoa Miami wakati zimebaki sekunde 1:18 aliporuka pembeni ya court na kutumbukiza mpira...Strategy ya Spurs mwishoni iliwakosesha nafasi ya kushinda kwani walitakiwa wacheze foul lakini hawakufanya hivyo na Bosh akapataa nafasi ya kutoa pasi na Spurs wakafungwa 98-96...Bofya hapa upate mambo zaidi...

Saturday, 7 June 2014

F1: NICO KUONGOZA GRID KESHO


Canadian GP ya kesho itaongozwa na Nico Rosbeg akifuatiwa na mwenzake Lewis Hamilton...Wa tatu ni Vettel, wa 4 ni Bottas na wa 5 ni Massa...

FRENCH OPEN: MARIA SHARAPOVA BINGWA


Maria Sharapva ameshinda mashinda michuano ya tennis ya French Open upadne wa wanawake kwa kumfunga Simona Halep...Mechi ilikuwa kali sana na lakini Sharapova ambae anatoka Urusi aliweza kukomaa na kushinda...Maria alimfunga Simona 6-4 6-7 (5-7) 6-4...Sharapova sasa meshinda vikombe vikubwa (Grand Slam) vitano na amekuwa wa 11 duniani kushinda vikombe vikubwa na yuko sawa na Martina Hingis...Sharpova amekiri mechi hii ni mechi ngumu amewhi kucheza ya Grand Slam...

Friday, 6 June 2014

FOSSIL RIDGE: SALIM JUMA ZONGO A.K.A BRING THE MONEY HOME

Cheki dogo Salim Juma Zongo mbongo anavyowatesa huko Marekani hapo chini kama 'Wide Receiver' akiwa anaichezea timu yake ya zamani ya shule ya Fossil Ridge...


TEXAS A&M: PATA PICHA ZA DOGO SALIM JUMA "BRING THE MONEY HOME" ZONGO MTANZANIA ANAYETESA MAREKANI

Hapa akimlisha uncle wake Rashid Mchujuko keki mwaka 2001
Dogo akipiga pozi na uncle Rashid Mchujuko


Mambo ya QB...Akimruka mtu mbioni kufunga bao

Dogo Zongo a.k.a Bring the money home ameshinda mara kibao...Kabati limejaa balaa...

Yuko na timu yake hapa...

Akiwa na mshkaji wake baada ya gaame za Oil Bowl...

Hapa anajaribu kumtoka mpinzani...


Hapa yuko na uncle Rashid Mchujuko ambae alimlea dogo Marekani...
Rashid na Zongo alipotembele Tanzania mwaka jana...




Timu ya Zongo inaitwa Panther...Wanamtegemea sana Zongo kama QB (Quarterback)   



Picha zimetolewa kwa hisani ya Rashid Mchujuko...

VPL: MBEYA CITY YAPATA MDHAMINI




Mbeya City timu ambayo imepta umaarufu mkubwa sana kutokana na uimara na umakini katika soka sasa imepata mdhamini rasmi...BINSLUM kampuni ya matairi na uwauzaji wakubwa wa battery za magari a RB ndio mdamini rasmi wa timu ya Mbeya City...Mbeya City ambayo iko chini ya Halmashauri ya Mkoa wa Mbeya imefurahi na kushukuru sana kupata mdhamini rasmi na hayo alisema Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri Dr. Samwel Lazaro mbele ya Mkurugenzi wa BINSLUM Mohamed Binslum wakati walipokutana na waandishi wa habari huko Mbeya...Bofya hapa upate habari zaidi...

WORLD CUP 2014: BEATS BY DRE WATOA TANGAZO KALI


Kampuni ya Beats By Dre iliyoanzishwa na mwanamuziki na producer mkali sana kutoka Marekani, Dr. Dre, na kununuliwa na kampuni ya Apple Inc kwa bilioni 3 dola za Marekani imeanza kutoa matangazo ya Beats By Dre kwa jina la 'Before the Game'...Tangazo moja hapo chini limehusisha wachezaji ma staa kutoka sehemu mbalimbali duniani...Hebu pata hilo tangazo kwa maa ya kwanza kutoka Max Sports...


NBA: GAME YA KWANZA YA FAINALI YA NBA KATI YA SPURS NA MIAMI

 

Tazama game ya kwanza ilivyo kuwa hapo juu...Spurs walishinda game 1...Game ya 2 itakuwa jumapili...Msikose kuangalia...

NBA: SPURS WACHUKUA GAME YA KWANZA YA FAINALI ZA NBA


Spurs jana waliweza kuchukua game ya kwanza ya fainali za NBA huko San Antonio...Spurs na Heat wanakutana tena kwenye fainali toka mwaka jana...Mwka jana walipambana sana mpaka game 7 na wachezaji wale wa mwaka jana ndio hao wa mwaka huu...


Game ilikuwa kali lakini kulitokea tatizo  la umeme ambalo lilifanya wachezaji wacheze kweye joto sana kwani AC zote hazikufanya kazi hapo AT&T center...LeBron James alitoka kukaa mara mbili kutokana na hali hiyo...San Antonio walishinda 110-95...Bofya hapa upate habari zaidi...

Thursday, 5 June 2014

WORLD CUP 2014: ENGLAND YASIMAMISHWA NA ECUADOR



Ecuador wameisimamisha England katika mechi kali ambayo tuliona kadi nyekundu 2 zikitolewa...Mechi iliisha 2-2...Defense ya England ilikuwa mbovu na Ecuador walichukua nafasi hiyo na kuachika bao mapema kutoka kwa Enna Valencia dakika ya 8....Lakini badae England walijipanga na Rooney akapachika bao dakika ya 29...Hili ni bao la 39 la Rooney kuifungia nchi yake...Lambert ambae amechukuliwa na Liverpool kwa pound za Uingereza milioni 4 aliwaweka England mbele kwa bao zuri dakika ya 51...Substitute Michael Arroyo alisawazisha kwa mkwaju mkali sana...


Oxlade-Chamberlaine aliumia goti na atahitaji kwenda hospitali akaangaliwe na wataalam...Kadi nyekundu zilitolewa na refa baada ya Sterling kumkwatua Valencia...Valencia alipewa kadi kutokana na jinsi alivyo lalamika....Bofya hapa upate habari zaidi...

Tuesday, 3 June 2014

EPL: LAMPARD AONDOKA CHELSEA


Frank Lampard ametangaa anaondoka Chelsea baada ya kukaa na club hiyo miaka 13...Lampard mwenye umri wa miaka 35 ndio mfungaji bora na anamagoli 211...Kwa sasa Lampard yuko Miami na squad ya England wakujitayarisha na World Cup...Amesema hato ongea kuhusu issue zake za mpira mpaka atakapotoka Brazil...Lampard alinunuliwa kwa pounds za Uingereza milioni 11 na amekuwa mtu wa 3 katika historia ya Chelsea katika idadi za game alizojitokeza kucheza...Lampard amecheza mechi 648 amepitwa na Ron Harris 795 na Peter Bonetti 729...Chelsea watamkumbuka sana Lampard na amesema Chelsea ilikuwa kama kipande cha maisha yake...Bofya hapa usome zaidi...

FRENCH OPEN: RATIBA YA MICHUANO YA LEO

Philippe Chatrier (13:00 UK start)

Seed Player
Player Seed Competition
  Muguruza Blanco (Spa) v Sharapova (Rus) Women's Singles
Raonic (Can) v Djokovic (Ser) Men's Singles

Suzanne Lenglen (13:00 UK start)

Seed Player
Player Seed Competition
14  Suarez-Navarro (Spa) v Bouchard (Can) 18  Women's Singles
Berdych (Cze) v Gulbis (Lat) 18  Men's Singles

Court 1 (10:00 UK start)

Seed Player
Player Seed Competition
Kubot (Pol)Lindstedt (Swe) v Golubev (Kaz)Groth (Aus)   Men's Doubles
Hsieh (Tpe)Peng (Chn) v Black (Zim)Mirza (Ind) Women's Doubles
Barty (Aus)Dellacqua (Aus) v Errani (Ita)Vinci (Ita)   Women's Doubles
11  Benneteau (Fra)Roger-Vasselin (Fra) v Gonzalez (Arg)Monaco (Arg)   Men's Doubles

Court 2

Seed Player
Player Seed Competition
  Parra Santonja (Spa)Gonzalez (Mex) v Groenefeld (Ger)Rojer (Ned)   Mixed Doubles
Shvedova (Kaz)Soares (Brz) v Mladenovic (Fra)Nestor (Can) Mixed Doubles

BOXING: FLOYD MAYWEATHER AACHANA NA GOLDEN BOY PROMOTIONS


Baada ya CEO wa Golden Boy Promotions, Richard Shaefer, kuachia ngazi kambi ya Mayweather Promotions kupitia CEO wao Leonard Ellerbe wamesema hawatafanya tena kazi na Golden Boy Promotions.

Monday, 2 June 2014

KUMBUKUMBU: SIKU KAMA YA LEO MARCO BARRERA ALIMTWANGA TOLEDO



Tarehe 2 June 1995 Marco Antonio Barrera (The babyface assassin) alichapa Frank Toledo knockout round ya 2 mara 2...Toleda aliendelea kuwa bingwa wa dunia badae...Enjoy hilo pambano hapo chini...

WOMENS FA CUP FINALS: TIMU YA WANAWAKE YA ARSENAL YANYAKUA KOMBE


FA Cup ya wanawake imemalizika kwa timu ya Arsenal kuchukua kombe tena...Arsenal iliichapa Everton 2-0 katika mechi ambayo ilikuwa rahisi sana kwa timu ya wanawake ya Arsenal...Kelly Smith alianza kuona lango la Everton mapema na badae alipata nafasi ya kumsukumizia Yukari Kinga mpira na hatimaye kupachika goli...Bofya upate habari zaidi...

Sunday, 1 June 2014

MOTO GP ITALY: MARQUEZ ASHINDA KWA MARA YA SITA


Marc Marquez ameshinda Italian GP na ni ushindi wa 6 mfululizo...

FRENCH OPEN: FEDERER NJE


Roger Federer ametupwa nje ya michuano mikali sana ya French Open...Mwaka huu tumeona mastaa wengi wakitolewa na madogo...Federer amechapwa na Ernests Gulbis....Huyu dogo ana mbwembwe sana na mara nyingine ana bamiza racquet yake chini...Gulbis mwenye miaka 25 ni namba 18 duniani...Bofya hapa upate habari zaidi...

AFCON: TANZANIA YASONGA MBELE



Tanzania imesonga mbele kwenye michuno ya awali yakufuzu kwenda African Cup of Nations 2015 baada ya tutoka sare 2-2 na Zimbabwe huko Harare leo joni...Tanzania wamepita kwa tofauti ya magoli 3-2...Habari njema kwa watanzania wengi....

MASHINDANO YA MBUZI: RATIBA (07/06/2014)


BOXING: CARL FROCH AMCHAPA GROVES



George Groves alisimamishwa round ya 8 mbele ya mashabiki 80,000 (haijawahi kutokea Uingereza) katika pambano kali la marudino...Sasa Froch ni bingwa wa mikanda ya WBA na IBF ya uzito wa middleweight...Hili pambano ni la marudino baada ya pambano la kwanza kuisha kwa malalamiko...


Froch alichapa sana Groves round ya 8 mpaka akaanguka na kuzimia kwa muda mfupi ndipo refa aliposimamisha pambano...Sasa Froch inasemekana atapambana na bingwa wa Olympics James DeGale...Bofya hapa upate habari zaidi...