Showing posts with label Oklahoma Thunder. Show all posts
Showing posts with label Oklahoma Thunder. Show all posts

Wednesday, 25 May 2016

NBA PLAYOFFS 2016: OKLAHOMA THUNDER YAINYAMAZISHA GOLDEN STATE WARRIORS KWA KUONGOZA 3-1


Hali si shwari kabisa ndani ya kambi ya Golden State Warrior kutokana na kujikuta wakiwa chini games 3 kwa 1 dhidi ya  OKC au Oklahoma Thunder...Thunder walisinda Game 4 118-94 na pongezi ziende kwa Russell Westbrook ambae aipata triple-double ya kihistoria...Westbrook alipata points 36, assists 11 na rebounds 11...Kevin Durant alipata points 26 na rebounds 11...Pamoja na Golden State kuweka historia katika regular season Thunder wamewakimbiza na kuonyesha kiu ya ushindi toka game ya kwanza ya playoffs...Bofya hapa upate habari zaidi.

Monday, 9 May 2016

NBA PLAYOFFS: KEVIN DURANT AISAIDIA THUNDER KURUDI LEVEL


Hali haikuwa safi kwa Oklahoma Thunder kwani kuna wakati walikuwa nyuma zaidi ya points 10 na kila wakijaribu San Antonio Spurs wanawazengua...Game 4 ilikuwa muhimu sana kwani Spurs wamesimama na wanacheza kikapu cha ukweli lakini Kevin Durant ilibide ajiongeze sana ili kukabiliana na San Antonio Spurs na Thunder wakafanikiwa kushinda 111-97...Kevin Durant alimaliza Game 4 akiwa na points 41...Sasa series iko sare 2-2 katika 'best of seven' series...Bofya hapa upate habari zaidi.

Friday, 4 March 2016

NBA: GOLDEN STATE WARRIORS WAFIKIA REKODI YA CHICAGO BULLSYA KUTOFUNGWA NYUMBANI MECHI 44


MVP Stephen Curry na timu yake ya Golden State Warriors wameifikia rekodi ya enzi za wakina Michael Jordan na Chicago Bulls ya kutochapwa nyumbani...Golden State waliwachapa Oklahoma Thunder 121-106 na kufikia rekodi hiyo...Curry kwenye hiyo game aliibuka na points 33 na mwenake Kevin Durant aliibuka na points 32...Chicago Bulls walishinda mechi 44 za nyumbani kuanzia March 30, 1995 mpaka April 4, 1996...Msimu huo wa 1995-96 Bulls walishinda game 72 ambayo ni rekodi katika NBA na Golden State wako njiani kuifukuzia hiyo rekodi...Bofya hapa upate habari zaidi.

Tuesday, 1 March 2016

NBA: STEPHEN CURRY APIGA GAME MOJA HATARI SANA


MVP Stephen Curry alipiga game moja hatari na kuokoa timu yake kwa kupiga shot moja very impossible...Golden State Warriors walishinda kwenye overtime baada ya Curry kupachika basket akiwa nje kabisa ya D...


Basket hiyo iliyoshinda game iliwashangaza wadau wa basket na pia wahasimu wake ambao wamembeza hivi karibuni...Wabaya wake wanasema eti anacheza hivyo kutokana na kuwa NBA haina wachezaji wa defense wazuri na pia wachezaji wa sikuhizi mayai na hawana nguvu ya kumsimamisha lakini aliwanyamazisha katika game hiyo dhidi ya Oklahoma City...


Kwa sasa Curry ndio anayeongoza ligi kwa kuwa na wastani wa points 30.7 msimu huu...Bofya hapa upate habari zaidi.

Friday, 18 December 2015

NBA: LeBRON JAMES AMUUMIZA MKE WA JASON DAY



Katika hali ya kawaida ya kuokoa mpira usitoke nje ya court, LeBron James, alifanikiwa kuokoa mpira lakini shida ni kwamba alimwangukia mke wa Jason Day na kumuumiza...Jason Day ni Professional Golfer huko Marekani na alikuwa amekaa pembeni yake wakiangalia game wakiwa court side...


Mke wa Jason anaitwa Ellie Day aliwekwa kwenye machela na kukimbizwa hospitali haraka...Ilikuwa game kati ya Cleveland Cavaliers na Oklahoma Thunder...Kwa sasa Ellie Day anaendelea vizuri...Bofya hapa upate habari zaidi.