Saturday, 2 April 2016

F1: HAMILTON KUANZA MBELE BAHRAIN GP KESHO


Lewis Hailton ataanza mbele kwenye grid baada ya kumaliza mbio za qualifying kwa kuweka rekodi ya lap huko Bahrain...Nico Roseberg atakuwa wa 2 na Sebastian Vettel atakuwa wa 3...Bofya hapa upate habari zaidi.

EPL: ARSENAL YAIZAMISHA WATFORD 4-0


Arsenal F.C wametoka kuwachapa Watford 4-0 hivi punde tu...Arsenal walikuwa kwenye form nzuri na walimiliki mpira muda mrefu pamoja na pasi za uhakika nyingi...Manabo yalitoka kwa Sanchez mapema dakika ya 4, Iwobi dogo kutoka Nigeria ambae aliingia academy akiwa na miaka 9 alifunga dakika ya 38, Bellerin nae alipachika bao dakika ya 48 na substitute Theo Walcott alifunga dakika ya 90...Bofya hapa upate habari zaidi.

Friday, 1 April 2016

AZAM SPORTS FEDERATION CUP: YANGA NA AZAM WASONGA MBELE


Azam wamesogea mbele kwenye kombe la ASFC baada ya kuwachapa Mbeya Prisons 3-0 ndani ya viwanja vya Chamazi...Yanga nao wameshinda mechi yao thidi ya Ndanda F.C. 2-1 ndani ya Uwanja wa Taifa...Stand United ya nao wameingia nne bora baada ya kuwazamisha Geita 3-0...Bofya hapa upate habari zaidi.

MIAMI OPEN: NICK KYRGIOS AINGIA NUSU FAINALI KWA MARA YA KWANZA


Nick anayetoka Australia amefanikiwa kufunga namba 12 duniani Milos Raonic na kuingia nusu fainali ya michuano mikali ya Miami Open Masters...Nick sasa ameweza kuwa namba 20 kwa ukali wa tennis duniani...Alishinda mechi kwa score ya 6-4 7-6 (7-4) na sasa watakutana na Kei Nishikori kutoka Japan...Bofya hapa upate habari zaidi.